Sunday, September 21, 2014

PETIT MAN AMUOA DADA WA DIAMOND PLATNUMZ


Meneja wa Mirror na wasanii wa Endless Fame, Petit Man (kushoto) akimvalisha pete ya ndoa dada yake na Diamond Platnumz aitwaye Esma usiku wa kuamkia leo.
Wanandoa wakiwa katika pozi baada ya kufunga ndoa.
Mama mzazi wa Diamond Platnumz na Esma, Sanura Kassim 'Sandra' (katikati) akiwa katika pozi na wanandoa hao.
Wanandoa Petit Man na Esma wakiwa katika picha ya pamoja.

Meneja wa Mirror na wasanii wa Endless Fame, Petit Man, amefunga ndoa ya Kiislamu na dada wa msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz aitwaye Esma usiku wa kuamkia leo.

MSANII BONGO FLEVA AAIBISHA MA-MISS



Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva aliyewahi kutamba na Kundi la Chamber Squad na ngoma yake ya taifa ya Kama Vipi, Moses Bushagama ‘Mez B’ anadaiwa kuwaaibisha ma-miss kwa kuwalazimisha kupiga nao picha wakiwa watupu.

Msanii wa kitambo wa Bongo Fleva wa Chamber Squad Moses Bushagama, ‘Mez B’ akijiachia na 'totoz' fukweni.

Tukio hilo la kidhalilishaji na lisilovumilika lilijiri juzikati kwenye Ufukwe wa Mikadi uliopo Kigamboni jijini Dar muda mfupi baada ya jamaa huyo ‘kushuti’ video ya ngoma yake mpya ya Shemeji.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, jamaa huyo aliwafuata warembo hao waliojitambulisha kwa majina ya Vicky na Rebecca waliokuwa kwenye swimming pool (bwawa la kuogelea) ambao ilisemekana kuwa siyo raia wa Bongo na huko wanakotokea ni ma-miss.
Ilidaiwa kwamba Mez B ndiye aliyewaomba kupiga nao picha lakini jamaa huyo ‘akaharibu’ baada ya kwenda mbele zaidi na kuanza kuwaminya ‘vifuu’ vyao kifuani vilivyoonekana ni vya saa sita vilivyokuwa wazi bila hata ‘braa’.


Ilisemekana kwamba baada ya kupiga picha hizo, yeye (Mez B) aliwafowadia washikaji zake ndipo zikazagaa kupitia mtandao wa WhatsApp.
“Hawa wasanii wetu kweli ni majanga. Ona Mez B alichokifanya na hawa mabinti. Yaani wapo kama walivyozaliwa lakini yeye yupo freshi na nguo zake. Kama siyo kudhalilishana ni nini! Amewaaibisha sana. Lakini na wao hawakuona?” alihoji mrembo mmoja aliyefowadiwa  picha hizo na rafiki yake kwenye WhatsApp.
Baada ya kuzitia picha hizo kibindoni, gazeti hili lilimtafuta Mez B kisha kumbana kuhusu tukio hilo ambapo alijitetea kwa ufupi:“Wale ma-miss walikuwa wanaogelea vifua wazi kwa muda mrefu. Wao ndiyo walioniomba kupiga nao picha.”
Kumekuwa na kasumba ya kupiga picha za utupu kisha kuziachia mtandaoni kwa kudhani kuwa ni kujiongezea umaarufu lakini ukweli ni kujiondolea utu na heshima mbele ya jamii.






Monday, September 8, 2014

JIHAN DIMESH AWA REDD’S MISS ILALA 2014


  Jihan Dameshi akiwa na mshindi wa pili Nasreen Abdul (kushoto)na Happiness Sostheen.
    …Wakijitayarisha kumtangaza mshindi.
    Majaji wakifuatilia shindano hilo.
      Warembo wakitoa ‘machejo’ kuonyesha umahiri wao katika ‘kudensi’.
   Mshiriki namba nane akiwa katika pozi la nguvu.
   Baadhi ya washiriki watarajiwa wa shindano la Miss Tanzania 2014 wakiwaangalia wenzao wa Ilala wakichuana.

  Jaji mkuu wa shindano la Miss Tanzania, Patel (kushoto) akiwa na familia yake katika shindano hilo.
    Baadhi ya warembo waliohudhuria katika shindano hilo.
    Martini Kadinda akiwa katika zulia jekundu.
   Waimbaji wa kundi la Yamoto Band wakiwa na kiongozi wao, Said Fella ‘Mkubwa na Wanawe’, na mmoja wa waratibu wa shindano hilo aliyejulikana kwa jina moja la Juma.
Muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’  akiwa kwenye zulia jekundu.
Miss Njombe 2014 naye alikuwepo.

    Martin Kadinda na Lulu.

MREMBO JIHAN DIMESH juzi usiku aliibuka Redd’s  Miss Ilala 2014 katika kinyang’anyiro kilichofanyika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam na kushirikisha wanyange kumi.
 

MADAWA YA KULEVYA: DIAMOND KIMENUKA



NIkweli kimenuka! Mbongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ yupo kikaangoni, habari zinadai kwamba kila anaponyanyua miguu, kikosi cha kupambana na kuzuia madawa ya kulevya nchini chini ya kamishna wake, Godfrey Nzowa nao wananyanyua miguu yao kumfuatilia, Amani limesheheni.

Mbongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akipozi.

Habari za kiintelijensia zilidai kwamba, kisa cha kikosi hicho kufanya hivyo kinadaiwa kuwa, serikali inamhofia kujihusisha na biashara hiyo haramu ya kusafirisha madawa ya kulevya ‘unga’ nje ya nchi kwa kutumia kivuli cha kwenda kufanya shoo.
Akizungumza na wanahabari wetu jijini Dar, Jumatatu iliyopita, afisa mmoja wa ngazi ya juu wa kitengo hicho ambaye hakupenda kuchorwa jina gazetini, alisema Diamond amepewa maelekezo yote muhimu.

MAELEKEZO ALIYOPEWA

“Tumempa maelekezo Diamond, atuletee mikataba ya shoo zote anazokwenda kuzifanya nje ya nchi ili tujiridhishe kama kweli ni halali au anakwenda kwa ajili ya biashara nyingine.
“Hiyo yote inatokana na uchunguzi wetu kwake kuhusu akaunti zake za benki kuonesha kwamba ana fedha nyingi sana zinazotia shaka kama amezipata kihalali,” alisema afisa huyo.
‘Diamond Platnumz’ akiwa kazini.
KUNUNUA NYUMBA
Afisa huyo aliendelea kusema kwamba, uchunguzi wao pia umebaini kwamba, msanii huyo wa Bongo amekuwa akinunua nyumba kila anaporejea kutoka kwenye shoo zake nje ya nchi, jambo ambalo taasisi haiamini kama kweli analipwa pesa nyingi kwa shoo moja, kiasi cha kumwezesha kununua nyumba jijini Dar.
“Tumebaini kwamba Diamond kila akirudi nchini kutoka kwenye shoo zake hununua nyumba. Analipwa kiasi gani cha fedha kule kwenye shoo? Hapa ndipo tunaposimamia sisi,” alisema afisa huyo huku akigongea msumari kuwa Diamond mwenyewe amekatazwa kuzungumza kwenye vyombo vya habari kuhusu kutakiwa kuwasilisha mikataba ya shoo zake za nje.
 KUNA UKWELI?
Amani lilifuatilia na kubaini kwamba, Diamond aliporejea kutoka kwenye safari yake ya Marekani hivi karibuni, alinunua nyumba kwa Sh. milioni 80 iliyopo maeneo ya Mwananyamala-Magengeni, Dar.
Siku za nyuma, msanii huyo aliwahi kuripotiwa kununua nyumba zaidi ya mbili maeneo ya Kijitonyama, Dar, kiasi cha kuandikwa na vyombo vya habari kwamba amenunua mtaa.
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa.
KUHUSU AKAUNTI YA BENKI

Diamond mwenyewe aliwahi kuhojiwa katika Kipindi cha Take-One kinachorushwa hewani na CloudsTV ambapo alipoulizwa akaunti yake inasomaje, alijibu kuwa ina zaidi ya bilioni moja hivi.

DONDOO ZA UWEZO WA DIAMOND

1. Ana utajiri unaozidi shilingi bilioni 1.
2. Yupo kwenye mazungumzo na promota wa Rwanda kufanya shoo moja ya uwanjani ambayo anaweza kulipwa dola 120,000 (zaidi ya Sh. milioni 190).
3. Malipo ambayo hupokea kwa shoo zake nyingi za nje ya nchi hayashuki chini ya dola 25,000 (zaidi ya Sh. milioni 40).
4. Tangu mwaka 2011 mwishoni akaunti yake haijawahi kushuka chini ya Sh. milioni 100.
5. Anamiliki nyumba kadhaa jijini Dar ambazo amepangisha watu.
6. Ili kuvunja mkataba na aliyekuwa meneja wake, Papa Misifa ilibidi amlipe Sh. milioni 18.
NZOWA AZUNGUMZA NA AMANI
Gazeti hili lilimtafuta Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Nzowa ambapo alipopatikana na kuulizwa, alisema:
Sehemu ya madawa ya kulevya yaliyowahi kukamatwa.
“Ni kweli! Sisi kila mtu mwenye kipato cha kutia shaka lazima tumchunguze. Diamond kama ana mali zote kwa nini tusimchunguze. Ikithibitika anajihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya ama zake ama zetu huo ndiyo utaratibu wetu.”

DIAMOND SASA

Amani lilimsaka Diamond na kumuuliza kama analijua kasheshe hilo ambapo alisema:
“Najua, ila nimegundua kuna watu wamepanga kunishusha chini kisanii ndiyo wanaoeneza taarifa kwamba mimi nasafirisha unga.”
Amani: Sasa unadhani kwa nini hao watu unaosema wamependa kukushusha kisanii wasitumie njia nyingine, hasa ya sanaa wakatumia hiyo ambayo unasema si kweli?
Diamond: We elewe hivyo kaka (akakata simu).

SAFARI ZA NJE

Kwa kipindi kirefu sasa Diamond ambaye ni mpenzi wa Wema Isaac Sepetu, amekuwa akisafiri nchi mbalimbali kwa shoo na mambo binafsi ambapo mbali na nchi kibao za Bara la Afrika, ameshasafiri nchi nyingi zikiwemo Marekani, Uingereza, China, Norway, Ujerumani, Dubai na nyinginezo.

Stori: Shakoor Jongo

AJALI YA GARI YAUA MBEZI JIJINI DAR

Mwili wa mwanamke mmoja ambaye hakufahamika jina lake baada ya kukanyagwa na lori na kupoteza maisha.
Msamalia mwema akiufunika mwili wa mwanamke huyo.
Baadhi ya wananchi wakiwa eneo la ajali.
MWANAMKE  mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja amepoteza maisha baada ya kukanyagwa na lori lenye namba za usajili T277 CLY leo katika maeneo ya Mbezi Tanki Bovu, jijini Dar es Salaam.

KESI YA PONDA YAAHIRISHWA MPAKA SEPTEMBA 22

Shehe Ponda akiwasalimu waumini ndani ya mahakama.
…Akiwa  na askari magereza.
Waumini wa dini ya Kiislam wakitoka Mahakama Kuu.
Askari magereza wakimtoa  Ponda mahakamani.
Gari la magereza lililompakia Shehe Ponda likitoka eneo la mahakama.
Wafuasi wa Shehe Ponda wakiwa nje ya mahakama.
KESI inayomkabili Shehe Ponda,  iliyokuwa inasikilizwa katika Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam, imeahirishwa tena  baada ya mawakili wa pande zote mbili kutakiwa kupeleka hoja  zao za utetezi kwa maandishi.
Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 22 Septemba mwaka huu. Aidha Shehe Ponda aliwaasa  waumini wanaomuunga mkono watume wawakilishi wachache kesi hiyo itafanyika katika chumba maalum kijulikanacho kama ‘chamber court’.

YALIYOJIRI MAHAKAMA YA MWANZO KINONDONI LEO


Watuhumiwa wakishushwa kwenye gari la Jeshi la Magereza, tayari kwa kusomewa kesi zao mahakamani.
Mmoja wa watuhumiwa  akiwa amebebwa na watuhumiwa wenzake kuingizwa mahakamani, haikujulikana mara moja sababu za kubebwa huko kwani askari walikataza kuwasogelea.

MWANDISHI wa mtandao huu, leo alinasa matukio kadhaa katika Mahakama ya Mwanzo ya Kinondoni, ambapo alishuhudia watuhumiwa  wa makosa  mbalimbali  wakiingizwa mahakamani hapo kwa ajili ya kusomewa mashitaka yao.